Nitaonana Na Yesu

 


1. Nitaonana na Yesu, uso kwa uso kweli,
Siku ile shangwe tele, nikimwona Mwokozi.


Kiitikio:
Tutaonana kwa macho, huko kwetu mbinguni,
Na kwa utukufu wake, nitamwona milele.


2. Sasa siwezi kujua, jinsi alivyo hasa,
Bali atakapokuja, nitamwona halisi.


3. Mbele yake yafukuzwa, machozi na huzuni,
Kipotovu kitanyoshwa, fumbo litafumbuka.


4. Uso kwa uso hakika, pale pale furaha,
Nitafurahi kabisa, nikimwona Mwokozi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *