Njia yote naongozwa

 


1. Njia yote naongozwa kwa mukono wa Mwokozi;
Ninaona wema wake, sina shaka wala woga,
Nina raha ya mbinguni, na salama tamu sana,
Na katika mambo yote ananitendea mema.
Na katika mambo yote ananitendea mema.


2. Njia yote naongozwa, ninategemea Yesu;
Anilinda jaribuni, ananipatisha nguvu.
Nikiona kiu hapa, nikichoka kwa safari,
Ninapata maji mengi toka Mwamba wa milele.
Ninapata maji mengi toka Mwamba wa milele.


3. Njia yote naongozwa kwa mapendo yake bora;
Ananituliza sana na ahadi yake nzuri.
Nitafika kwake mbingu kufurahi kwa milele,
Nitaimba neno hili, Yesu aliniongoza.
Nitaimba neno hili, Yesu aliniongoza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *