Nmeitaji Mwokozi

 


1. Nimehitaji Mwokozi
Awe nami daima;
Nataka mikono yake,
Kunizunguka sana.


Ref
Hofu rohoni sina,
Aniongoza tena;
Sitanung’unika tena,
Nimfuate daima.


2. Nimehitaji Mwokozi,
Sina imani nyingi;
Atanifufusha moyo,
Wengine hawawezi.


3. Nimehitaji Mwokozi,
Mwendoni mwa maisha;
Katika mateso mengi,
Tena katika vita.


4. Nimehitaji Mwokozi,
Kiongozi njiani;
Kwa jicho aniongoze,
Ni’fike mbinguni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *