Baada Ya Kazi na tabu zote
Baada ya kazi na taabu zote
Nikiingia kwenye furaha,
Kumwona Yesu, Kumwabudia,
Kutakuwa furaha yangu kuu.
Ref
Kumwona tu ni furaha,
Kumwona tu ni furaha
Nikiondolewa shida zote,
Nikiona uso wa Bwanangu.
Mwenye rehema anipendaye,
Akinipa Kikao mbinguni.
Nitamfurahia mponya wangu,
Kwa kumwona tu uso kwa uso.
Pale mbinguni kwenye furaha,
Nitaonana na ndugu wengi
Lakini kumwona Bwana Yesu,
Kutakuwa furaha kabisa.